0


Sababu kubwa za mvua kuathiri miundombinu ni udhaifu na uongozi mbovu wa serikali ya Dar es salaam. Naelekeza haya matatizo Dar kwa sababu Moshi Kilimanjaro hayapo.
Ktk maisha yangu, kitu ninachokichukia kupita vyote ni kuona mtu mwenye akili zake anatupa takataka ovyo
Mtu ananunua miwa harafu anatafuna huku anatupa ovyo ovyo. Mtu anatupa anavyojisikia kutupa apendavyo. Takataka za majumbani zinatupwa kwenye madaraja ovyo.
Viongozi wanakimbilia kwenye kuzuia pikipiki kuingia mjini wkt hatari ipo kwenye utupaji wa takataka ovyo.
Ukichunguza madhara ya utupaji taka, sidhani kama serikali inaweza kushindwa kuzuia hili tatizo. Binafsi naona ni uzembe wa hali ya juu.
Leo tunaona wananchi hao hao nyumba zao zimejaa maji. Mitaro imeziba, maji yanabadili njia.
Tuanze na tuchukue hatua. Sema NO na "NO" kwenye mkono unao ruhusu kutupa takataka.

Kwa mfano angalia picha zifuatazo,,,







Serikali ya Jiji la Dar es Salaam ndo tatizo,inaongoza kwa mazoea???????????amkeni usingizini mtunge sheria na kuzisimamia ni marufuku mtu kutupa taka ovyo ukidhibitika umetupa taka ovyo fine,, plus sero sku mbili tosha kabisa kwa kuanzia.

Post a Comment

 
Top