0
Incoming President Muhammadu Buhari























Abuja;

Rais mteule wa Naijeria Muhammadu Buhari kashutumu madai Boko Haram ya kuwa kundi la kidini kuwa ni upotoshwaji, Rais mteule ameeleza kwamba atapambana vikali dhidi ya wanamgambo wa Kiislam.

"Wadanganyifu hawa waitwao Boko Haram wanaweza kushindwa na kutokomezwa kabisa kwa kuangamiza ngome zao za mafunzo,huu ni mradi wao tu wenywewe wamejiajiri sasa wanatumia dini, Hakuna dini inaruhusu mauaji ya watoto katika mabweni ya shule, katika masoko na maeneo ya ibada.," Alisema.

"Hawana dini inayowafanya wawe hivyo, hawa ni magaidi na sisi tutakabiliana nao kama tunavyo kabiliana na magaidi."

Buhari, alishinda uchaguzi wa rais mwezi uliopita kwa ahadi ya msimamo mkali dhidi ya Boko Haram, ambao ni waasi inakadiriwa watu takribani elfu 15 wameshaa uawa tangu 2009 na kuanza zaidi ya million moja na nusu 1,500,000 bila makazi.

mtawala huyo wa zamani wa kijeshi alimtuhuhu mpinzani wake Rais Goodluck Jonathan kwa kushindwa kuongoza katika kukabiliana na tishio la usalama wa taifa ilo.

Hakuna kitu kibaya ambacho mtu anaweza kufanya kama kukataza watoto kupata elimu,hiyo itakuwa kuwaharibia watoto maisha ya baadae.
Buhari ambaye atatawazwa kuwa Raisi rasmi mei 29, ametahadharisha kuwa hawezi kuahidi kuwa atawaokoa na kuwarudisha salama watoto 219 waliotekwa nyara zaidi ya mwaka sasa.

Lakini yeye ameahidi kusaidi maeneo yaliyo kumbwa na vurugu na kunyimwa haki za kijamii na uchumi yaendelee na mipango ya maendeleo.

Taarifa hii ilitolewa na chama chake cha All Progressives Congress (APC)


Post a Comment

 
Top