0

John ni kijana mwenye umri wa miaka 30.
Ana shahada ya uzamili (Masters) ktk
masuala ya Usimamizi wa biashara, na
kwa sasa anafanya kazi kama Mkurugenzi
wa fedha kwenye shirika moja la
kimataifa hapa nchini.
Hajaoa bado, lakini ana nyumba mbili
nzuri za kuishi hapa jijini. Moja Mbezi
Beach na nyingine Kimara.. Ana gari 2 za
kutembelea na 3 za biashara.. Anamiliki
duka moja la nguo Kariakoo na jingine la
simu Mlimani city.. Ni mcha Mungu,
mpole na mtanashati.. Ni miongoni mwa
vijana waliofanikiwa kimaisha.
John ana rafiki yake aitwae Michael..
Huyu ni Afisa Mtendaji mkuu (CEO) wa
Shirika moja la ndege hapa nchini. John
na Michael wamekua marafiki kwa muda
mrefu.. tangu utotoni..
Wamekua pamoja, wamesoma pamoja
tangu chekechea hadi chuo kikuu. Hata
masomo yao ya juu (masters) walisoma
pamoja Marekani licha ya Michael kupata
ufadhili Australia, lakini alikataa kwenda
ili tu akasome na John Marekani.
Walipendana kama mapacha licha ya
kuwa hawakuwa ndugu wa damu..
Ukimkosea John umemkosea Michael and
its vice versa.!
Waliitwa mapacha walipokua shuleni kwa
namna walivyopendana. Kila mmoja
alimheshimu mwenzie na kila mmoja
alijitahidi asimkwaze mwenzie..
Kila mmoja amefanikiwa kutokana na
juhudi za mwenzie.. upendo wao ulikua
wa kweli kutoka kwenye vilindi vya mioyo
yao.. Walimpenda Mungu na wote
walikua viongozi wa jumuiya za vijana
makanisani mwao.
Baada ya kuona wamefanikiwa kimaisha
John akashauri watafute wenzi wa
maisha...that means waoe.. Michael
akasema anahofia kuoa kwa haraka kwani
anaweza kupata mke atakayeharibu
urafiki wao.. Mke asiyejua walikotoka na
hivyo kuleta mfarakano baina yao...
Akamshauri John wasubiri kwanza hadi
WAKATI WA BWANA ULIOKUBALIKA..
John hakumuelewa Michael kbs, na
akadai tayari ana mchumba na
anampenda sana.. Michael akamuuliza
kwa muda gani wamekuwa pamoja, John
akajibu miezi 6.
Michael akasema Miezi 6 haitoshi
kumchunguza mwenzi wa maisha lakini
John akasisitiza anampenda...
Mipango ya harusi ikafanyika na Michael
akachagua kuwa mwenyekiti wa kamati ya
harusi ya John.. Lengo lake likiwa
kusimamia harusi ya rafiki yake na
kuhakikisha inafanikiwa.
John akamshauri Michael "tafadhali nawe
tafuta mwenzi uoe ili usiwe mpweke. Ni
dhahiri sasa nitakua karibu zaidi na mke
wangu kuliko wewe. Majukumu ya
kifamilia nayo yatanibana, hivyo tafuta
mwenzi ili upunguze upweke..."
Michael akajibu "Nimemuomba Mungu
anipe mke atakayenifaa.. Bado nasubiri
jibu lake. Siwezi kuoa ili tu niepuke
upweke,.maana ndoa ni zaidi ya kuondoa
upweke.. Nahitaji mwenzi wa maisha,
sihitaji mtu wa kuniondolea upweke.."
Siku moja John akiwa katoka Michael
akampigia simu kuwa yupo nyumbani
kwake. John akamuomba amsubiri maana
yuko mbali kidogo ila atarudi.
Mke mtarajiwa wa John nae alikua
nyumbani kwake, hivyo John akamshauri
Michael apige story na shemeji yake hadi
atakaporudi.
Lakini John aliporudi nyumbani
hakumkuta Michael, akamkuta mchumba
wake analia.. alipomuuliza kulikoni
akasema Michael alijaribu kumbaka...
John akawaka kwa hasira... kwa kuwa
alimpenda sana mchumba wake na kwa
kuwa hakumkuta Michael nyumbani
akaamini maneno ya mchumba wake.
Akiwa amechanganyikiwa akaendesha gari
kwa kasi kwenda kwa Michael. Ile kufika
akamkuta Michael kajilaza kwenye sofa.
Lakini kabla hajamuuliza chochote,
akampiga kichwani na chupa ya mvinyo
aliyokua ameshika mkononi... Michael
akaanguka na kuzirai..
Akakimbizwa hospitalini ambako
ilionekana amepata athari kubwa ndani
ya kichwa hivyo alihitaji upasuaji..
John akiwa amefura kwa hasira akarudi
nyumbani kwa mguu na kuiacha ile gari
kwa Michael, maana alipewa zawadi na
Michael siku ya birthday yake.. hivyo
akamrudishia zawadi yake maana aliona
mtu aliyejaribu kumbaka mchumba wake
hawezi kumpa zawadi.
Kwa kuwa hakuwa na gari aliweza kuingia
hadi ndani bila mchumba wake kumsikia
wala kumuona... Alipofika akamkuta
anaongea na simu "yes Jenny
nimemkomesha.. atajuta kukukataa...Nim
emwambia John kuwa alitaka kunibaka,
John akawaka hasira na kwenda
kumfuata... najua huko ni kivumbi na
jasho na urafiki wao utaisha leo shosti..."
Alipomaliza kuongea na simu na kugeuka
akamuona John.. Akapanick maana
hakutegemea...
John akamwambia usiseme lolote maana
nimesikia yote.
Kumbe Jenny alikua rafiki yake mchumba
wa John.. Na alipenda kuolewa na
Michael lakini Michael alimkataa ili
kulinda urafiki wake na John.. sasa ile
hasira ya kukataliwa ndo wakapanga
kuwafarakanisha..
John alipojua ukweli akajilaumu sana kwa
maamuzi ya haraka aliyochukua.. akiwa
mnyonge,.na majuto moyoni akakimbia
hospitalini ili akamuombe Michael
msamaha.
Alipofika akakutana na nesi akamzuia..
John akapaza sauti huku akibubujikwa na
machozi "tafadhali naomba niruhusiwe
nikamuombe Michael msamaha.. Najua
amepoteza fahamu na hawezi kunisikia.
Lakini naamini nafsi yake itanisikia na
kunisamehe kwa ukatili niliomtendea..
Ooh Michael my friend urafiki wetu wote
nimeshia kukupeleka ICU..Nisamehe
Michael sikujua..."akalia kwa uchungu
John.
Mara daktari akatokea. John kwa shauku
akamuuliza "dokta Michael
anaendeleaje??"
Daktari akamuangalia John kwa huruma
kisha akasema, "Nasikitika kukujulisha
kuwa Michael amefariki dakika chache
zilizopita baada ya damu nyingi kuvujia
kwenye ubongo.."
Kisha akaongeza "tumejitahdi kwa kadri
ya uwezo wetu kuokoa maisha yake lakini
imeshindikana.."
John akakamatwa na kutupwa gerezani
anakotumikia kifungo cha maisha..
MORAL OF THE STORY..!
Kuwa makini unapotafuta mwenzi wako
wa maisha. Wengi huharibu mahusiano
yao na rafiki zao, ndugu zao au wazazi
wao kisa wameoa/kuolewa.
Usiruhusu mke/mume awe chanzo cha
uadui kati yako na ndugu zako, wazazi au
rafiki zako.
Ukiona mke/mume ni chanzo cha uadui
na ndugu zako ujue huyo mke/mume ana
roho ya mfarakano (spirit of confusion).
Pilli, unapopata tatizo kwenye mahusiano
kuwa na subira.. Usiharakie kufanya
maamuzi.
Mara zote maamuzi ya haraka
humgharimu mtu baadae. Ona John ktk
umri mdogo wa miaka 30, anaenda
kumalizia gerezani maisha yake yote
yaliyobaki hapa duniani.
Mali zake, elimu yake, cheo chake,
heshima yake na vyote alivyovijenga
maishani ni kazi bure, just for a single
mistake.
Bila shaka huko gerezani alipo
anatamani siku zirudi nyuma ili afanye
maamuzi mbadala lakini haiwezekani
tena... Itz over and out..!!
Mungu akubariki unayesoma ujumbe
huu. Kama umeoa/kuolewa amuondolee
mwezi wako Spirit of Confusion, na kama
hujaoa upate mke/mume asiye a spirit of
confusion.
Upate mtu atakayewapenda rafiki zako,
ndugu zako na wazazi wako na
kuwathamini..
Kumbuka "asiyewapenda wa kwao ni
mbaya kuliko asiyeamini.."
Hivyo muombe Mungu umpate
atakayewapenda wa kwenu. 

Stay
blessed.!!


Post a Comment

 
Top