0
Baada ya kuwaza sana...nimegundua jiji lote la Dar ni sehemu ya bahari. Bado historia haijanithibitisha ila naamini mwanzoni mwa karne ya 16 jiji hili lilikuwa bahari...Kutokana na kukua na maendeleo ya Dunia unaoendana na uharibifu wa mazingira ulipelekea maji ya bahari kusogea na kurudi nyuma taratibu kwa zaidi ya karne 2...kuondoka kwa maji hayo kuliacha ardhi ikiwa tupu na baada ya miaka mingi baadae binadamu wakalikuta eneo lililo pembezoni mwa bahari. Jamii hiyo ya watu kutoka bara wakaweka makazi eneo hili na kuanzisha familia na kutokana na kujitenga kwao kwa miaka mingi, wakajikuta wanatengeneza mila na desturi zao ndipo wakajiita jamii ya Wazaramo. Wazaramo limetokana na mtazamo wa kusema jamii yao ilitengwa...hivyo ilidharauliwa..ndipo wakasema 'Waza + ramo'
Uthibitisho wa Nadharia hii.
1.Kuwepo na mafuriko kila mahali linalolikumba jiji hili ni jambo linaleta usahihi wa mtazamo wangu.
2.Kuwepo na vilima na miunuko iliyopo pembezoni mwa mkoa wa Dar es salaam kama vile Pugu,Mbezi n.k...miunuko ni sifa ya bahari.
3.Jiji la Dar es Salaam sehemu kubwa ni tambarare na hakuna udongo eneo lote la Dar ni michanga.
4.Kupitiwa kwa mwamba wa bahari ardhini....hii inathibitishwa popote unapochimba kisima katika sehemu yoyote ya Dar unapata maji.

Post a Comment

 
Top